Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Chaneli ya 14 ya Israel imeripoti Kikao cha Timu ya Serikali ya Utawala wa Kizayuni (Israel) kilichofanyika kwa Njia ya on-line wakiwa katika Miji tofauti ndani ya Ardhi ya Palestina (inayokaliwa kimabavu na Utawala haram wa Kizayuni) kwa sababu ya hofu na wahka wa kuogopa Makombora hatari ya Iran.
Sehemu ya viungo wa timu ya Baraza la Amani ya Israel pia wameonekana wakiwa na Netanyahu kwenye Kikao hicho cha on-line, ambapo walikuwa katika sehemu moja wapo ya kujificha chini ya Ardhi kwa ajili ya Amani yao wakiogopa Moto wa Makombora ya Iran.
Hivi sasa, kwa ujumla utaratibu wa vikao vya serikali hii ya Kizayuni ni chini ya ardhi.
Wakati huo, Serikali ya Iran inaendelea na shughuli zake kama kawaida bila kujificha mapangoni chini ya ardhi. Na huu ndio utofauti Mkubwa uliopo baina vita vya Imani na Ukafiri, na Daima Imani hushinda Ukafiri.
Your Comment